Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Laurent Fabius amejiuzulu wadhifa huo . Bwana Fabius ambae pia aliwahi kuwa Waziri Mkuu ameteuliwa kuwa Rais wa Baraza la Katiba la Ufaransa.
Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Laurent Fabius
Maafisa wa serikali nchini Ufaransa wamethibitisha leo kwamba Waziri Fabius amejiuzulu wadhifa wake na kwa maana hiyo ameamua kujiondoa kwenye siasa za mstari wa mbele baada ya kuwamo katika medani hiyo kwa miaka zaidi ya 30.
Bwana Fabius alionekana akiwapungia watu wakati alipokuwa anatoka kuhuduhuruia kikao chake cha mwisho cha baraza la mawaziri leo asubuhi. Mwenyewe amethibitisha kwamba amejiuzulu wadhifa wake, hatua itakayosababisha kufanyika mabadiliko ya baraza la mawaziri baadae mnamo wiki hi
No comments